Jumatatu , 25th Aug , 2014

Wasanii na wanamitindo mbalimbali nchini Kenya wanatarajia kuungana kwa pamoja kufanya onesho maalum la Harambee kwa kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwasaidia watu waliopatwa na ugonjwa wa Saratani.

msanii wa muziki Alisha Popat

Onesho hilo lililobatizwa jina 'Fushion Night' litafanyika jijini Nairobi mnamo tarehe 13 mwezi Septemba mwaka huu litawahusisha wanamitindo na wasanii nyota wakiwemo Dan 'Chizi' Aceda, Alisha Popat, Wanny Angerer na Cindy Ogana.

Aidha wanamitindo ambao wataonesha mavazi yao mbele ya jukwaa wamo Kiko Romeo, John Kaveke, na wengineo wengi.