Jumanne , 3rd Mei , 2016

Baada ya fununu kuzagaa juu ya msanii anayetamba kutoka lebo ya Wasafi Raymond Tip Top kuwa ndiye msanii anayeibeba lebo hiyo meneja wake Ricardo Momo amefunguka juu ya fununu hizo.

Msanii kutoka lebo ya Wasafi RayMond Tiptop

Akikanusha fununu hizo Ricardo alisema kuwa si kweli kwakuwa kila msanii katika lebo yao huwa anajitungia nyimbo yeye mwenyewe "labda kusaidiana tu kimawazo".

“Hakuna anayemuandikia mwingine ila wanasaidizana wote kwa pamoja kila mtu ana uwezo wake na kila mtu anajiamini kwa kile anachokifanya”, alisema Ricardo.

Fununu zilizopo mitaani ni kuwa msanii Raymond ndiye muandishi wa nyimbo nyingi zadi katika lebo hiyo mpaka ngoma ya Bado iliyoimbwa na Harmonize ambayo alipokonywa na kupewa Harmonize.

Ricardo aliongeza kuwa awali wasanii hao wote nyimbo zao zilikuwa na jina moja la 'Bado' na wao wakaona haifai ndiyo wakaamua kutofautisha majina na kuita 'kwetu' na 'Bado'.