Jumatatu , 21st Feb , 2022

Hiltan Kalugho mwenye umri wa miaka 94, amerejea nyumbani kwao nchini Kenya mikono mitupu baada ya kupambana Tanzania kutafuta maisha kwa miaka 42 bila mafanikio.

Mzee Hiltan Kalugho

Kalugho alirudi Kenya wiki iliyopita na kuambiwa mkewe alifariki mwaka 2007, na watoto wake wawili kati ya saba wamefariki.

Kalugho aliondoka Kenya mwaka 1980 na kumuacha mkewe na watoto saba na kuingia nchini Tanzania kutafuta maisha.