Alhamisi , 9th Feb , 2017

Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona, Luis Suarez amedai kuwa ana matumaini ya kwamba rufani yake itakayokatwa itaweza kumuokoa asikose mchezo wa fainali ya Kombe la Mfalme baada ya kutolewa kwa kadi nyekundu katika mchezo wa nusu fainali.

Luis Suarez

Suarez aliifungia Barcelona bao katika mchezo huo dhidi ya Athletic Bilbao ambao ulishuhudia wachezaji watatu wakipewa kadi nyekundu na kumalizika kwa sare ya bao 1-1 iliyofanya Barcelona kufuzu fainali ya nne mfululizo kwa jumla ya mabao 3-2.

Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina alitolewa nje kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka mitatu aliyokaa Barcelona baada ya mwamuzi kudhani kuwa alimpiga kiwiko Koke katika dakika za majeruhi.

Suarez amesema kadi hiyo aliyopewa inamfanya ajisikie kucheka kwani inaonekana kama mwamuzi alidhamiria kufanya hivyo, na kusema kuwa wanataka kuona kama wanaweza kukata rufaa kwasababu hadhani kama alifanya kosa lolote kustahili adhabu hiyo.