Wakurugenzi wa ufundi wa vyama vya mikoa, wametakiwa kuwanoa vijana wa mchezo wa baiskeli ili kurahisha kazi kwa kocha wa timu ya Taifa ya mchezo huo.
Mwenyekiti wa chama cha baiskeli Tanzania (CHABATA), Godfrey Mhagama, amesema vijana wakifundishwa mapema itakuwa kazi rahisi kufundisha vijana hao na si kupandisha viwango.
Tanzania inajiandaa na mashindano maarufu ya baiskeli ya Tour of Rwanda, yatakayofanyika mwezi Novemba mwaka huu, nchini Rwanda.