Kombe la mashindano ya Carabao la nchini England.
Arsenal walipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya AFC Wycombe, Tottenham Hotspurs wakiwatoa Wolves kwa penalti 3-2 baada ya sare 2-2 dakika 90 wakati ambao Leicester City ilishinda 2-0 Milwall.
Baada ya matokeo hayo droo ya Carabao ilipangwa usiku wa kuamkia leo ambapo Westham United wamepangwa na Manchester City wakati Chelsea wamepangwa kucheza na Southapton Wanderers.
Droo ya hatua ya 16 bora ya kombe la Carabao inataraji kuchezwa Oktoba 25 hadi 26, 2021.