Juma Kaseja
Akiongea kwenye mahojiano kabla ya mchezo jijini Kigali, Kaseja amesema wao wameshafanya maandalizi yote lakini wanaamini mwalimu atakuwa anatazama zaidi mchezo ujao.
''Mimi nafikiri mchezo utampa nafasi kocha wetu kujua tunaingiaje kwenye mchezo dhidi ya Sudan hiyo Oktoba 18, 2019, sisi tumejiandaa vizuri nawaomba tu watanzania watuombee tufanye vizuri', - amesema.
Kwa upande wake kocha msaidizi Suleiman Matola amesema kuwa wanauchukulia kwa umuhimu wote mchezo huo, na kwamba kwasababu unapigwa siku ya kumuenzi Baba wa taifa, watafanya kila namna ili kushinda mchezo huo.