
Kiungo wa Yanga, Tonombe Mukoko akiwa mazoezini na kambi ya timu hiyo iliyopo nchini Morocco.
Bumbuli amesema, “Alikuwa na tatizo la kiafya ambalo lilimuweka nje yeye pamoja na Abdallah Shaibu 'Ninja' kwa siku tatu tangu wafike Morocco, lakini baada ya kufanyiwa tathmini leo ameruhusiwa kufanya mazoezi ya jioni pamoja na wenzake".
Baada ya Bumbuli kusema hayo, Mukoko mwenyewe amefunguka kwa kusema alikuwa anasumbuliwa na kichwa lakini kwa sasa yupo sawa na anaendelea na mazoezi. “Tumekuja hapa, nilikuwa naumwa kichwa kidogo, sasa hivi iko fresh mimi iko hapa na Yanga sasa hivi”.
Kwa upande mwingine, Kiungo mpya wa Wanajangwani, kutoka Uganda, Khalid Aucho anatazamiwa kujiunga na kambi leo Agosti 20, 2021 wakati beki Yennick Bangala atajiunga na kikosi hicho kilichopo Morocco kwa sasa siku ya Jumamosi ya kesho Agosti 21, 2021.