Alhamisi , 12th Aug , 2021

Mchezaji mpya wa klabu ya Simba Peter Banda amekabidhiwa jezi namba 11 ambayo hapo awali ilikuwa ikitumiwa na Luis Miquissone ambaye anahusishwa kujiunga na miamba ya soka barani Afrika klabu ya Al Ahly ya huko Misri.

Picha ya Mchezaji Peter Banda na Luis Miquissone

Banda alijiunga na wekundu wa Msimbazi mwezi Agosti 3 mwaka huu akitokea Nyasa Big Bullets ya nchini Malawi kwa mkataba wa miaka mitatu.

Mabingwa hao wa Tanzania hivi sasa wapo nchini Morocco ambako wameweka kambi yao kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya ujao.