Uwanja wa Nelson Mandela
Uwanja huo unatarajiwa kutumika katika mchezo wa fainali ya kombe la Azam Sports Federation utakaohusisha timu ya Simba Sport Club na Namungo FC.
Akithibitisha hilo Mwenyekiti wa RUREFA Blass Kihondo, amesema wana Rukwa hawana sababu ya kuwa na wasiwasi tena kwani mtaalamu kutoka TFF amejiridhisha na kusema uwanja huo upo vizuri na tayari kwa kutumika Julai 2, 2020.
Ili kuepukana na udanganyifu na wizi wa tiketi Kiondo amesema wameandaa mpango mkakati mzuri ili kuhakikisha hautokei na mchezo utaanza na kumaliza vizuri.
Tazama Video hapo chini