Mbwana Samatta
Hiyo ni baada ya kuifunga timu ya taifa ya Uganda 'The Cranes" kwa mabao 3-0, mabao yaliyofungwa na Simon Msuva, Erasto Nyoni na Aggrey Morris.
Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta ni miongoni mwa wachezaji waliocheza kwa kiwango cha juu katika mchezo huo, mara baada ya kumalizika kwa mchezo alikwea pipa na kurejea Ubelgiji katika klabu yake ya Genk huku akiacha ujumbe mzito kwa Watanzania.
Katika ukurasa wake wa Instagram, Samatta ameandika,
Samatta alivyoondoka baada ya kazi
Pia wakati anaondoka katika Uwanja wa Ndege wa JNIA kuelekea Ubelgiji, majira ya saa 7 za usiku, Samatta aaliandika ujumbe, "mpaka wakati ujao, ahsanteni sana", ukionesha kuwa yuko safarini kurejea klabuni kwake.
Taifa Stars imeungana na timu ya taifa ya Uganda, Kenya na Burundi zitakazoiwakilisha Afrika Mashariki katika michuano ya AFCON itakayofanyika kuanzia mwezi June hadi Julai, 2019 nchini Misri.
Bonyeza hapa chini kutazama zaidi.







