Thomas Mueller
Muller amesema kucheza na timu ya wachezaji wa ridhaa, kwenye mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia, kuliiweka Ujerumani, kwenye hatari ya kuumia, huku pia Mtendaji Mkuu wa klabu ya Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge, akisema kuwa San Marino haifanyi kitu kwenye soka la kulipwa.
Waziri wa Utalii na Michezo wa San Marino, Teodoro Lonfernini, ametaka kuombwa radhi kwa maneno hayo, na kusema Ujerumani ni mabingwa wa dunia, lakini siyo wakubwa wa dunia.
