Mhe. Mchengerwa amefafanua kwamba Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria na imeanza kuwezesha wasanii kimitaji ili kuboresha maisha yao.
Aidha, amesema wiki ijayo Serikali itatoa mikopo ya awamu ya pili baada ya Ile ya mwanzo iliyotolewa mwishoni mwa mwaka jana.
Ameongeza kuwa katika tukio hilo pia Serikali itapokea mdundo wa taifa na vazi la Taifa kutoka kwenye Kamati za kitaifa alizoziteua kufanya kazi hizo.