Yanga na Pyramids
Yanga imeangukia katika kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kuondolewa katika hatua ya pili ya Klabu Bingwa Afrika na Zesco United ya Zambia, ambapo imepangwa na matajiri wanaokuja kwa kasi kutoka nchini Misri, Pyramids FC wakianzia nyumbani.
"Tunawamudu, kwanza Pyramids ni timu mpya ina miaka 11 tu na tunafahamu kuwa msimu uliopita mpaka kufikia walipo walimaliza nafasi ya tatu", amesema Hassan Bumbuli.
"Ni timu yenye uwekezaji mkubwa na ina pesa nyingi sana lakini pamoja na uwekezaji huo sisi tunaangalia kiwango cha uchezaji uwanjani", ameongeza.
#MICHEZO Wapinzani wa Yanga kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, Pyramids FC waliasisiwa upya mwaka 2018 baada ya kununuliwa na Mwenyekiti wa Shirika la Michezo la Saudia, Turki Al Sheikh.
Huu ni msimu wa kwanza kwa klabu hiyo kucheza michuano ya vilabu barani Afrika. pic.twitter.com/op3RH7YAEq
— East Africa TV (@eastafricatv) October 10, 2019
Yanga itaanzia nyumbani kucheza na timu hiyo, Oktoba 27 katika Uwanja wa Taifa kabla kurudiana Novemba 3 nchini Misri.