Alhamisi , 18th Nov , 2021

Timu ya taifa ya Soka la Ufukweni Tanzania inataraji kucheza dhidi ya Mozambique kwenye mchezo wao wa ufunguzi wa michuano ya COSAFA saa 6:30 Mchana wa leo Novemba 18, 2021 nchini Afrika Kusini.

(Kikosi cha timu ya taifa ya soka la Ufukwenu Tanzania 2021)

Baada ya mchezo huo wa ufunguzi, Tanzania itashuka dimbani tena leo saa 10:30 jioni kucheza dhidi ya Comoros kwenye mchezo wa pili wa siku ya Ufunguzi na endapo itapata alama nyingi basi itafuzu hatua ya mtoano inayofuata.

Tanzania ipo kundi B na timu za Mozambique na Comoros wakati wenyeji Afrika Kusini wapo kundi A na timu za Angola, Madagascar na Visiwa wa Seychelles.

Michuano hiyo imeanza kutimua vumbi Jumatano ya Jana Alhamisi Novemba 17 na kutaraji kutamatika Jumapili ya Novemba 21, 2021.