Jumapili , 9th Apr , 2017

Shirikisho la Soka Tanzania TFF, limetangaza kufanya Mkutano wake Mkuu siku ya Jumapili ya Agosti 12, 2017.

Maamuzi hayo yamefanyika katika kikao cha Kamati ya Utendaji cha Shirikisho hilo, kilichokutana  leo Jumapili Aprili 9, 2017 ambapo miongoni mwa ajenda katika mkutano huo, itakuwa ni uchaguzi mkuu wa TFF.

Kwa mujibu wa Katiba, uchaguzi huo utachagua Rais wa TFF, Makamu Rais wa TFF na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji.