Jumanne , 21st Oct , 2025

Klabu ya soka ya Yanga imetangaza kuwa hakutakuwa na kiingilio katika mchezo wao wa ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Silver Strikers ya Malawi mchezo utakaopigwa Oktoba 25 katika dimba la Benjamini Mkapa Dar es Salaam.

Prince Dube

“Uongozi wa Yanga SC umekubaliana mechi ya Jumammosi ambayo itakuwa mechi ya maamuzi itakuwa ni bure isipokuwa jukwaa la VIP A  na jukwaa la VIP B haya  yatakuwa maalum kwaajili ya wageni waalikwa” Ally Kamwe Meneja wa Habari na mawasiliano Yanga SC

Katika mchezo wa awali Yanga walipoteza kwa kichapo cha Go;o moja kwa sifuri dhidi ya mabingwa wa nchini Silver Strikers matokeo yaliyokuwa tiketi kwa aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Romain Folz

Yanga wanahitaji kuchinda mchezo wa marudiano utakaopigwa Oct 25 Siku ya Jumamosi katika dimba la Benjamin Wiliam Mkapa ili kupata tiketi ya Kufuzu hatua ya makundi katika kombe la Ligi ya Mabingwa Barani Afrika