Afisa Habari wa Azam FC, Zakazakazi
Akifanya mahojiano maalumu na EATV & Radio Digital, Zakazakazi amesema mipango yao ya msimu huu ni kumaliza nafasi ya pili kwakuwa Simba SC tayari imeshabeba ubingwa huku akiweka wazi sababu iliyopelekea wao kukosa ubingwa kuwa ni kutokana na kubadilishwa kwa makocha.
Azam FC itajitupa dimbani kesho majira ya Saa 1:00 Usiku katika mtanange wa Robo Fainali ya Kombe la shirikisho dhidi ya Simba SC.