Jumatano , 2nd Nov , 2016

Kocha wa Timu ya Taifa ya mchezo wa Tenisi walemavu Riziki Salum amesema mashindano ya wazi yatakayoishirikisha nchi ya Kenya yatasaidia kuinua vipaji vya wachezaji wake ambao wanajiandaa na kalenda ya mwakani.

Tennis walemavu

 

Kocha wa mchezo huo Riziki Salum amesema, mashindano hayo ambayo yatakuwa ya mwisho kwa mwaka huu yatasaidia wachezaji wake kuwaandaa kwa mashindano ya Kenya pamoja na ya Afrika Kusini huku akiitaka Serikali na wadau wa mchezo huo kuisaidia timu hiyo na vifaa mbalimbali vya mchezo huo hususani viti ambavyo vitawasaidia katika mashindano hayo.

Kocha Riziki amesema, iwapo serikali na wadau watajitokeza kusaidia mchezo huo, katika mashindano ya mwakani wanaamini watafanya vizuri zaidi kwani hawatakuwa na changamoto nyingi kama ilivyo kwa mwaka huu ambapo wamejitahidi katika mashindano mbalimbali licha ya changamoto walizonazo.