
Kushoto ni Dj Msabato, kulia ni Nay wa Mitego
Dj Msabato amesema jambo hilo lilipelekea kukwazana na 'boss' wake ambapo kulitokea tofauti kati yao hadi alipoamua kuacha kufanya kazi pamoja.
"Kuna mwanamke wangu alitaka kumuiba nikawa sijapenda hilo suala baada ya kumfuata akawa anabisha wakati kuna message zilikuwa zinaonekana kwamba ni kweli alikuwa anamtongoza mwanamke wangu ambaye nilimchagua, nilijaribu kumwambia lakini alikuwa anakataa nikaamua kutoka ili tusifikie pabaya" amesema Dj Msabato
Tumejaribu kumtafuta Nay wa Mitego kwa njia ya simu lakini bahati mbaya hakuweza kushika simu yake ili kujibu madai ya tuhuma hizo.