Jumamosi , 8th Oct , 2022

Mikoa ya kanda ya ziwa inaelezwa kuwa hatarini kugeuka kuwa jangwa kutokana na kupoteza zaidi ya asilimia 50 ya uoto wa asili suala linalosababishwa na uharibifu wa mazingira unaoambatana na shughuli mbalimbali za binadamu ikiwemo ujenzi wa makazi pamoja na shughuli za uchimbaji wa madini.

Picha ya jangwa

Hayo yamebainishwa jijini Mwanza na Meneja wa wakala wa misitu TFS kanda ya ziwa, Bakari Salim  baada ya zoezi la upandaji miti lililoambatana na utoaji wa taulo za kike katika shule ya sekondari ya wasichana lugeye iliyopo wilayani Magu shughuli iliyoratibiwa na shirikisho la walimu Mkoa wa Mwanza na kusema kuwa ili kuinusuru Mikoa hiyo ipo haja ya kupanda miti mingi.

kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Adam Malima ameahidi kufanya zoezi la upandaji miti kuwa endelevu ili kukabiliana na changamoto hiyo ya ukame katika maeneo mbalimbali Mkoani humo.