Jumatano , 14th Dec , 2022

Jumla ya wanafunzi 1, 073, 941 waliofaulu mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2022 wakiwemo wavulana 514, 846 na wasichana 559, 095 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2023

Taarifa ya TAMISEMI imeeleza kuwa Idadi ya wanafunzi waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza Januari, 2023 imeongezeka kwa wanafunzi 166, 139 sawa na ongezeko la asilimia 18.30 ikilinganishwa na Wanafunzi 907, 802 waliopata alama ya kujiunga na Kidato cha kwanza mwaka, 2022

Kati waliofaulu na kupangiwa kujiunga na kidato cha kwanza wamo wanafunzi wenye mahitaji maalum 2, 775 sawa na asilimia 0.26 ambao kati yao wavulana ni 1, 491 na wasichana 1, 284