
Godbless Lema
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji Mkuu wa Idara hiyo SSI. Paul Mselle, imesema kwamba utaratibu uliotumika kumzuia Lema kutoka nchini ni wa kawaida na unatumika kwa raia yeyote pale ambapo Idara imepata taarifa zinazohitaji mhusika kuhojiwa.
"Aidha, Idara ya Uhamiaji inatoa wito kwa wananchi kupuuza taarifa za uongo zilizochapishwa na ndg. Lema kupitia mitandao ya kijamii kuwa zuio hilo linawalenga viongozi wote wa CHADEMA," imesisitiza taarifa hiyo.