Kulingana na uamuzi huo, Vizcarra alipokea hongo sawa na $676,000 kutoka kwa makampuni ya ujenzi badala ya kandarasi za kazi za umma alipokuwa gavana wa eneo la kusini la Moquegua kuanzia 2011 hadi 2014.
Wakati wote wa kesi hiyo iliyoanza Oktoba iliyopita, Vizcarra alikanusha mashtaka hayo, akidai alikuwa mwathirika wa mateso ya kisiasa.
Aliingia madarakani mwaka wa 2018 baada ya mtangulizi wake kujiuzulu na akafukuzwa miaka miwili baadaye na Bunge huku kukiwa na uchunguzi wa ufisadi.
Timu yake ya wanasheria ilithibitisha kuwa imekata rufaa dhidi ya hukumu hiyo, ambayo pia ilimpiga marufuku Vizcarra kushikilia ofisi ya umma kwa miaka tisa.
Kaka yake mkubwa, Mario Vizcarra, anapanga kugombea katika uchaguzi wa rais wa Aprili 2026 kwa chama cha "Peru Kwanza", ambapo rais huyo wa zamani amewahi kuwa mshauri mkuu.
Timu yake ya wanasheria ilithibitisha kuwa imekata rufaa dhidi ya hukumu hiyo, ambayo pia ilimpiga marufuku Vizcarra kushikilia ofisi ya umma kwa miaka tisa.



