Mikoa inayoongoza kwa UVIKO-19 yatajwa
Wizara ya Afya imesema kumekuwepo na ongezeko la wagonjwa wa UVIKO-19 kutoka wagonjwa 8 katika wiki ya tatu ya mwezi Aprili hadi kufikia wagonjwa 32 katika wiki ya nne ya mwezi huo, huku mkoa wa Dar es Salaam ukiongoza kuwa na visa vya watu 70 waliothibitika kuwa na ugonjwa huo.