Tanzania U23 yapewa neno na Rais Samia
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameimwagia sifa za pongezi timu ya taifa ya Tanzania ya vijana chini ya miaka ishirini na tatu baada ya vijana hao kuliwakilisha taifa vema kwa kuwa mabingwa wa michuano ya CECAFA kwa msimu huu 2021.