Aggrey Morris kuagwa rasmi mechi ya Taifa Stars
Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF, limetangaza mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars), dhidi ya timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, utatumika kumuaga mchezaji Aggrey Morris ambaye ametangaza kustaafu kuitumikia timu ya taifa.