Taifa Stars kuweka kambi Misri, Mkude abaki
Kikosi cha wachezaji 20 wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania 'Taifa Stars' kinatarajiwa kuondoka kesho Jumanne saa 10.45 jioni kwenda Misri kufanya kambi ya siku nane kujindaa na mchezo dhidi ya Lesotho utakaofanyika Juni 10, 2017, Dar es Salaam.

