Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Amwagiwa maji ya moto kisa Fistula

Wednesday , 22nd May , 2019

Tafiti zinaonesha zaidi ya wanawake 800 Duniani hupoteza maisha kila siku kutokana na matatizo yatokanayo na ujauzito ambapo 20 kati yao wananapata majeraha au ulemavu na moja ya majeraha makubwa wakati wa kujifungua ni tatizo la fistula ya uzazi. 

Picha wa wakina mama wanaotibiwa Fistula katika hospitali ya CCBRT jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo Mwakilishi kutoka Shirika la idadi ya watu Duniani (UNFPA) Felister Bwana amesema kuwa mimba za utotoni, huduma duni za afya ni chanzo kikubwa cha ugonjwa huo kwa nchi za kiafrika.

"Inakadiriwa kwamba wanawake na wasichana zaidi ya milioni mbili wanaishi na tatizo la fistula duniani na hasa chini ya jangwa la Sahara", amesema Felister.

Www.eatv.tv imezungumza na baadhi ya wanawake wenye tatizo la Fistula ambao wanapatiwa matibabu katika hospitali ya CCBRT na wametoa ushuhuda wa namna walivyonyanyapaliwaa huku wakieleza hali zao kwa sasa baada ya kupata matibabu, Rehema Malugu kutoka mkoani Mara anaeleza kuwa ameishi na ugonjwa huo kwa miaka ishirini.

"Ugonjwa huu nimeishi nao kwa miaka 20, nimeteseka sana ndani ya ndoa nimemwagiwa maji ya moto na mume wangu, nimeachiwa alama ya maisha", amesema Rehema.

Kwa upande wake Rais wa chama cha madaktari wa Fistula nchini, Dkt. James Chapa, amesema kuwa ugonjwa huo unawaathiri wakina mama kiuchumi, kijamii na kisaikolojia.

Hayo yanajiri wakati Dunia ikijiandaa kuadhimisha siku ya kutokomeza fistula ambayo huadhimishwa Mei 23, aidha maadhimisho ya kutokomeza fistula duniani kwa mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu isemayo Fistula ni ukiukwaji wa haki za binadamu-tuitokomeze sasa.

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi