Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bajeti ya 2019/20 yawasilishwa na haya mapendekezo

Thursday , 13th Jun , 2019

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amesoma makadirio ya Bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/2020, bungeni leo Juni 13, 2019.

Waziri wa Fedha Dkt. Philip Mpango

Katika makadirio hayo Waziri mpango amesema jumla ya shilingi Tril 33.11 zinatarajiwa kukusanywa na kutumika katika bajeti ya mwaka 2019/20.

''Mapato ya ndani ni Tril 23.05 ambayo ni 69.6% ya bajeti yote. Mapato yatakayotokana na kodi ni Tril 19.10 sawa na asilimia 12% ya pato la taifa'' - Philip Mpango.

Baadhi ya michanganuo ya bajeti 2019/2020

Tril 7.56 Mishahara,
Tril 1.44 Umeme vijijini,
Bil 788.8  Reli, Maji, Usambazaji Umeme
Bil 450 Elimu ya juu
Bil 288.5 Elimu bure,
Bil 600 Wazabuni

Katika bajeti hiyo Waziri Mpango pia amependekeza kufutwa kwa msamaha wa kodi kwenye taulo za kike.
''Kufuta kwa msamaha kodi ya ongezeko la thamani kwenye taulo za kike kwa kuwa haujawezesha kupatikana kwa bei nafuu kwa bidhaa hiyo muhimu kwa walengwa, badala yake ni kuwanufainisha wafanyabiashara'', amesema.

Aidha amependekeza kutoza ushuru wa asilimia 10 kwenye bidhaa za nywele za bandia, zinazotengenezwa ndani ya nchi na asilimia 25 zinazoagizwa kutoka nje ya nchi, lengo ni kuongeza mapato ya Serikali.

Pia amependekeza kuongeza muda wa leseni ya udereva kutoka miaka 3 hadi 5, kuongeza tozo ya leseni 40000 hadi 70000, ada ya usajili wa magari 10000 hadi 50000, bajaji kutoka 10000 hadi 30000 na pikipiki kutoka 10000 hadi 20000.

Amesisitiza kuwa tozo zote zilizokuwa zinatozwa kwa dola za Kimarekani zitatozwa kwa shilingi ya Tanzania, isipokuwa kwa shehena za kemikali zinazokwenda nje ya nchi.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa