Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

CHADEMA Rukwa yatoa sababu za wanaohama

Wednesday , 15th Aug , 2018

Baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Rukwa kumfukuza diwani hivi karibuni na mwingine kujiuzulu leo, Mwenyekiti wa chama hicho mkoa huo Shadrack Malila maarufu Ikuwo amesema wengi wanaohama ni wasaliti wanarudi kwao.

Picha ya uzinduzi wa moja ya mashina ya CHADEMA na haihusiani na habari.

Akiongea na www.eatv.tv muda mfupi baada ya diwani wa Kata ya Mambwenkoswe wilayani Kalambo Kanowalia Siwale kutangaza kujiuzulu na kuhamia CCM, Malila amesema alijua hilo tangu mapema kwasababu amekuwa akimweleza mambo mengi ikiwemo kupata vitisho kutoka kwa viongozi wa juu wilaya.

''Wanaohama sio wanachama halisi wa CHADEMA na hawajui dhumuni la chama hiki kwahiyo wanapoteteleshwa na vitisho au hongo huwa wanaamua kusaliti na wengi wao huja na vijisababu vyepesi kama vitisho lakini mwisho wa siku ukifuatilia unagundua wanarudi walikotoka na huwa tunawabaini mapema ndio maana wengine tunawatimua'' amesema.

Aidha Malila ameongeza kuwa kuondoka kwa wanachama hao ambao ni wasaliti kunakiongezea uimara chama hicho kutokana na kubaki na wanachama ambao ni waaminifu na wanajua dhumuni na thamani ya chama hicho. Pia ameweka wazi kuwa wanaendelea na uchunguzi kwa baadhi ya madiwani wanaodaiwa kukisaliti chama na wakibaini hilo watatoa adhabu sitahiki.

Amemaliza kwa kusema kuwa kinachowafanya waamini kuwa viongozi wanaohama ni mamluki ni kitendo cha CCM kuwapa dhamana ya kugombea tena katika maeneo waliyotoka. Jumapili Agosti 12, CHADEMA mkoa wa Rukwa ilitangaza kumfuta uanachama diwani wa kata ya Majengo wilaya Sumbawanga Bw. Dickson Mwanandenje.
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala