Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Fatma Karume aomba radhi

Wednesday , 18th Apr , 2018

Rais mpya wa Chama cha wanasheria wa Tanganyika (TLS), Fatma Karume ameiomba radhi serikali kwa kutoa lugha kali ambazo zilizokuwa zinaenda moja kwa moja kugusa muhimili wa Mahakama kuhusiana na mambo ambayo yanayoendelea nchini kupitia Mahakama bila ya kufuata haki za kisheria

Fatma Karume ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa Zanzibar ametoa kauli hiyo leo Aprili 18, 2018 wakati akizungumza katika kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio kwa njia ya simu ambapo amesema zoezi la kuteua Majaji nchini liangalie zaidi taaluma za wanaoteuliwa badala ya kuwateua kwa mlengo wa kisiasa.

"Mahakama ni mhimili unaojitegemea hivyo ni vema ukaheshimiwa kwa kuchagua Mahakimu wenye vigezo vya kitaaluma ambao watasimamia vema sheria badala yakuyumbishwa na siasa. Mimi nipo tayari kushirikiana na serikali kwa sababu siwezi kutengeneza bajeti lakini naweza kushirikiana nao katika kuelezea mapungufu yaliyopo", amesema Fatma.

Mbali na hilo, Rais Fatma Karume ameweza kuweka wazi mipango yake ambayo atakayoweza kufanya katika kipindi cha uongozi wake.

"Kitu cha kwanza ni lazima tuifanye Mahakama iweze kufanya kazi zake katika weledi wake kwa hivyo watu wakiwa 'appointed' kuwa Majaji, Mahakimu. Tusiganye hizi 'appointed' kwa mujibu wa siasa lazima ziwe 'professional'. Inamaana kwamba unai-Professionalize Mahakama nzima, hiyo ni 'point' namba 'one' lakini namba mbili mishahara, unajua muda mwingine tunalalamika rushwa lakini unampa mtu laki nane ayaendeshe maisha yake lakini kesi inakuja ya milioni 200 ndani yake, lazima tuweze 'ku-balance' hivi vyote ni vitu muhimu sana maana tunasema tuna muhimili wa Mahakama lakini hatuwezi kujiendesha, hivi kweli muhimili unaweza kusimama? kusimama kwa ari!! na naomba msamaha hapa sababu nasema mambo, unajua saa nyingine unakuwa na hamasa na unaweza kusema mambo ambayo yana 'emotional", amesisitiza Fatma.

Kwa upande mwingine, Fatma Karume amesema kuna madhaifu mengi katika muhimili wa Mahakama ndani ya nchi hii na katika nyanja za sheria ambapo amedai changamoto nyingine ni miundombinu mibovu ya majengo ya Mahakama.

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari