Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Likizo ya uzazi ni mara 1 kwa miaka mitatu"

Wednesday , 18th Apr , 2018

Serikali ya awamu ya tano kupitia Wizara ya Nchi Ofisi ya Utumishi na Utawala Bora imesema haioni haja ya kubadilisha sheria iliyopo ya uzazi kwa sasa, kwasababu inampa fursa mwanamke kupumzika kutozaa mara kwa mara na kufuata uzazi wa mpango kama nchi inavyoelekeza nasio vinginevyo.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Wizara hiyo, George Mkuchika leo Aprili 18 Bungeni jijini Dodoma kwenye kikao cha 12 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalum Sonia Juma Magogo aliyetaka kufahamu mpango wa serikali wa kutaka kuwasaidia wakina mama ambao wanajifungua kabla ya kipindi cha kuruhusiwa kupata miezi mitatu ya mapumziko ili waweze kuwanyonyesha vichanga hivyo na kuendelea majugumu yao ya kiofisi ?.

"Kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma za mwaka 2009. Mtumishi wa umma anapojifungua hupewa likizo ya malipo ya siku 84 na iwapo atajifungua zaidi ya mtoto mmoja (mapacha) ataongezewa siku 14 na kuwa jumla ya 98. Endapo mtumishi atajifungua mtoto tena kabla ya kutimiza miaka mitatu atapewa likizo maalum ya wiki sita ili kuhudumia mtoto wake kwa mujibu wa kanuni na baada ya hapo serikali inaweza kumuongezea siku za kupumzika kulingana na ushauri wa daktari", amesema Mkuchika.

Pamoja na hayo, Waziri Mkuchika ameendelea kwa kusema "likizo ya uzazi hutolewa mara moja katika kipindi cha miaka mitatu kwa kuzingatia sera ya afya ya mama na mtoto inayosisitiza kulinda na kujenga afya ya mama na mtoto na kuhimiza uzazi wa mpango. Sheria hizi ni za nchi nzima hivyo zinapaswa ziheshimiwe na kufuatwa kwa wale waliokoa serikali na mashirika ya umma.

Kwa upande mwingine, Waziri George Mkuchika, ametoa rai kwa watumishi wa umma au sekta binafsi, kuwa endapo yeyote atakayenyimwa haki ya likizo ya uzazi basi aitaarifu Wizara husika ili hatua stahiki zichukuliwe kwa mwajiri wake.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala