Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Magufuli amteua mbobezi wa uhandisi

Thursday , 11th Oct , 2018

Rais Dkt. John Magufuli, leo Oktoba 11, 2018 amefanya uteuzi kwa kumteua Dkt. Dalmas Lucas Nyaoro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS). Uteuzi huo umeanza Oktoba 10, 2018.

Rais Magufuli

Dkt. Nyaoro ambaye ni mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), ana uzoefu wa zaidi ya miaka 30 katika sekta ya uhandisi wa masuala ya Ardhi na teknolojia, (Geotechnical) akiwa na uwezo mkubwa wa kutatua matatizo makubwa ya fani hiyo kwa kutumia ufumbuzi wa vitendo na kinadharia.

Amefanya kazi katika nyanja zote za uhandisi wa 'Geotechnical', pia ni mtaalam mzuri wa uhandisi wa udongo, muundo wa udongo tata, mbinu za uboreshaji wa ardhi na maeneo mengine mbalimbali ikiwemo upimaji wa udongo katika maabara.

Dkt. Dalmas Lucas Nyaoro

Nyaoro ni mbobezi wa masomo ya Hydrogeological akimiliki PhD na MSc katika mitambo ya udongo kutoka Chuo cha Imperial (UK). 

Pia ni mhandisi aliyesajiliwa na bodi ya wahandisi nchini, ambaye ni mwanachama wa Taasisi ya wahandisi Tanzania.
 

Taarifa ya Ikulu inaeleza zaidi hapo chini.

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari