Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mapya yaibuka Mbowe kupokonywa ofisi na DC Sabaya

Friday , 18th Jan , 2019

Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Hai linaloongozwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, Bi Irene Lema amekanusha taarifa ya kupokonywa ofisi ya Mbunge wa Jimbo hilo kama ilivyotangazwa na Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya hivi karibuni.

Mbunge wa Jimbo la Hai Freeman Mbowe

Kwa mujibu wa Katibu huyo Freeman wa Mbowe, hawajawahi kutumia ofisi yeyote iliyopo ndani ya Halmashauri ya Hai kutokana na Freeman Mbowe kuwa na wageni wengi huku chumba cha halmashuri kikishindwa kuhudumia idadi ya wageni wengi aliyokuwa nao.

Irene Lema amesema, "Mbunge hana ofisi ndani ya Halmashauri ya Hai, na aliamua kuweka nje ya halmashauri kwa sababu ilikuwa ni ndogo sana na akaamua kuweka nje ili kuwapokea wageni wengi wanatokea ndani na nje ya jimbo, hatujawahi kuitumia ofisi ambayo Mkuu wa Wilaya amesema amempokonya Mbunge."

"Ofisi yetu iko wazi muda wote na ninavyokwambia muda huu nimetoka kukutana na watu watatu ambao wanashida na Mbunge, kwa hiyo ofisi yetu tunashirikiana vizuri sana na wafanyakazi wote wa halmashauri ya Hai akiwemo Mkurugenzi tena bila kujali vyama vyao", ameongeza Irene Lema.

Mapema wiki iliyopita hii, Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya alitangaza kumpokonya Freeman Mbowe ofisi yake, akidai kuwa kiongozi huyo hajaonekana katika ofisi yake kwa muda mrefu.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala