Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Matendo ya polisi yamshangaza Katibu wa Mbunge

Monday , 18th Sep , 2017

Katibu wa Mbunge wa Tarime Vijijni John Heche, Mrimi Zabloni amesema analishangaa Jeshi la Polisi nchini kwa kukamata watu wanaokusanyika kumuombea Tundu Lissu na kuruhusu matamasha yanayofanyika usiku kucha huku viongozi wa mikoa wakishiriki.

Mrimi amefunguka hayo wakati akizungumza kwa njia yasimu na Mwandishi wa EATV na kusema kwamba anasikitisha na vitendo vinavyofanywa na jeshi la polisi kukataza mikusanyiko ya wanachadema badala ya kuipa ulinzi.

"Kuna vitu hawa askari polisi wetu wanafanya vya kushangaza, kuna matamasha mengi yanafanyika usiku na viongozi wa mikoa wanashiriki lakini maombi ya Lissu yanayofanywa mchana kweupe wanayapinga, sijui tunaelekea wapi. Kati ya matamasha ya usiku na maombi yapi yanahatarisha amani? Wenzetu Kenya jana wamefika hadi hospitalini na kufanya ibada kwa ajili ya kumuombea Lissu kwa nini hatujifunzi kutoka huko? alisisitiza kwa njia ya kuhoji.

Aidha Mrimi amewataka watu kutohusisha tukio la Tundu Lissu kama mtaji wa siasa kwa Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA) na kwamba harakati zinazofanywa na vijana hao ni kuhakikisha wanatoa hisia zao juu ya matatizo aliyoyapata mwanasheria wao.

Amesema kuwa wanachokifanya Bavicha siyo siasa bali wanatumia uhuru wa Katiba na kwa mujibu wa sheria ya vyama vingi nchini kwani wanaruhusiwa kuzungumza na hata kuandamana ili kutoa hisia zao kwa mambo yanayoendelea nchini.

"Wanaosema Bavicha wanamtumia Lissu kama mtaji wa kisiasa ni mtazamo wao tu, kwani naamini wanafanya kazi kwa mujibu wa heria na katiba hayo mengine ni hila tu. Naamini wamekumbwa na matatizo mengi viongozi kupotea, misukosuko ya viongozi wa chama lakini pia hata mauaji yaliyowahi kutokea kwa viongozi na shambulio la Lissu kwa hiyo ni haki yao kama vijana kupaza sauti kukemea" Mrimi aliongeza
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma