Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Mtazilipa Watanzania wote"- Rais Magufuli

Sunday , 2nd Dec , 2018

Rais John Magufuli leo Desemba 2, 2018 amezindua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa visima vikubwa vya maji zaidi ya 20 jijini Arusha.

Rais Dkt. John Magufuli.

Rais amesema kuwa mradi huo utakaogharimu shilingi bilioni 520, unahusisha visima vya kuchimbwa na kumaliza tatizo la maji katika Jiji hilo, na zimekopwa katika Benki ya Maendeleo ya Afrika, hivyo zitalipwa na Watanzania wote kupitia kodi.

"Serikali imekopa bilioni 520 kutoka Benki ya maendeleo ya Afrika, kwa ajili ya Arusha ili kutekeleza mradi wa maji, hizi hela zitalipwa na Watanzania wote, na tumezileta kwa wale wale wanaoitukana serikali, na yote ni kwasababu maendeleo hayana chama", amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Isack Kamwele kutosita kuwafukuza wakandarasi wakishindwa kutekeleza mradi huo kwa wakati, "Waziri usiogope kufukuza wakandarasi, kumbuka hata mimi nimewahi kuwa Waziri wa Ujenzi na sikusita kutimua wakandarasi wasiotekeleza miradi, wakaanza kuniombea laana, na hazikunipata kwakuwa Mungu anapenda maendeleo ya haki, wewe fukuza tu".

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amesema mradi huo ukikamilika uhaba wa maji Jiji la Arusha utapungua kwa kiasi kikubwa.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala