
Bwana Green ambaye alikuwa mshirika wa karibu wa Waziri mkuu Theresa May alibainika kuwa alitoa taarifa zisizo sahihi kuhusu picha za ngono zilizokutwa kwenye komputa yake ya ofisini.
Aidha Bw. Green alikuwa anachunguzwa pia juu ya madai ya kutowaheshimu wanawake wanaharakati katika chama chake cha Conservative.
Hata hivyo kiongozi huyo amekanusha kuhusika na mashitaka yote yanaomkabili.