
Taarifa hiyo imesema ndege hiyo MS804 ilikuwa na abiria 56 na watumishi 10, wakati ikitoweka.
Ndege hiyo ilikuwa angani umbali wa futi 37,000, wakati ilipotoweka mashariki mwa Mediterranean.
Shirika la ndege la Misri limesema litatoa taarifa zaidi litakapopata taarifa mpya kuhusu tukio hilo.