Habari zilizothibitishwa na Shirika la ndege la Ethiopia imesema kwamba ndege hiyo ilikuwa ikitoka Ethiopia kwenda Nairobi, ilipata hitilafu angani na kupelekea kuanguka kwake.
Shirika limesema tayari imeshatuma timu yake eneo la tukio ili kuokoa majeruhi kama wapo, na muda si mrefu watatoa namba za abiria waliomo ili ndugu zao waweze kuwatambua.
Serikali ya nchi hiyo tayari imeagiza vyombo vya usalama kwenda eneo la tukio, na kufanya lolote liwezekanalo kunasua miili na wajeruhi waliomo.