Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Nitakwenda kuwajua hukohuko CCM"- Pauline Gekul

Sunday , 14th Oct , 2018

Baada ya aliyekuwa Mbunge wa Babati Mjini (CHADEMA), Pauline Gekul kutangaza kujiuzulu wadhifa huo na kujiunga na CCM , amesema kuwa matabaka na kudharaulika ndani ya chama ndiyo sababu iliyopelekea yeye kukihama chama hicho huku akikiri kuwa hakifahamu vizuri chama hicho licha ya kuhamia.

Aliyekuwa Mbunge wa Babati Mjini (CHADEMA), Pauline Gekul.

Akizungumza na www.eatv.tv, Gekul ameeleza kuwa amefanya hivyo ili kutimiza wajibu kwa wananchi wake kwani anashindwa kuzitimiza ahadi hizo akiwa upande wa upinzani.

Gekul amezungumzia suala la kuwa huenda amelipwa pesa ili kujiunga na CCM, ambapo amesema kuwa "Sijanunuliwa na nina kwenda CCM nikiwa siwafahamu kabisa lakini nashukuru nimepata mapokezi mazuri na nitakwenda kuwajua huko huko, wala sijanunuliwa kama wanavyosema".

Gekul amesema kuwa amechoshwa na matabaka yaliyomo ndani ya CHADEMA, kutokusikilizwa na kuthaminiwa kwa baadhi ya watu na wengine akidai kuwa wanaonekana kama chaguo la tatu mbele ya viongozi.

Barua ya kujizulu kwa Gekul ilianza kusambaa kwa kasi mitandaoni jana, Oktoba 13, saa 4 usiku kwenda kwa Spika wa Bunge Job Ndugai, ambapo sasa anaungana na wengine waliojizulu hivi karibuni akiwemo, Mwarya Chacha (Serengeti) na James Milly wa Simanjiro, wote wa CHADEMA.

Gekul anakuwa Mbunge wa nane kujiuzulu kutoka upinzani kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) na kupewa nafasi ya kugombea tena nafasi hiyo, wabunge hao ni; Dkt. Godwin Mollel (Siha-CHADEMA) na Maulid Mtulia (Kinondoni-CUF) huku wanaosubiri kuapishwa ni, Mwita Waitara (Ukonga), Julius Kalanga (Monduli) na Zuberi Kuchauka (Liwale-CUF) ambaye aliibuka mshindi katika uchaguzi uliofanyika jana Jumamosi Oktoba 13,2018 kwa ushindi wa asilimia 85.

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi