Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Raila aweka mapumziko

Tuesday , 17th Oct , 2017

Muungano wa Upinzani nchini Kenya NASA umeahirisha maandamano yake dhidi ya tume ya uchaguzi nchini humo IEBC huku kukiwa na madai ya maafisa wa polisi kutumia nguvu zaidi dhidi ya waandamanaji ikiwa ni pamoja na kuua raia wasio na hatia.

Kiongozi wa upinzani nchini humo Bw. Raila Odinga amesema hatua hiyo imeafikiwa kufuatia vifo vya baadhi ya wafuasi wake ambao alidai walipigwa risasi na polisi na kuongeza kwamba muungano huo utatoa mwelekeo wake baada ya siku ya Mashujaa itakayofanyika Ijumaa .

Katika taarifa hiyo ya Odinga inadaiwa kumlaumu Waziri wa Usalama Fred Matiangi na Inspekta jenerali wa polisi Joseph Boinet akiwashutumu kwa kuwaagiza maafisa wa polisi kuua raia wasio na hatia.

"Kwa heshima ya wale waliouawa na serikali, maandamano yetu yataahirishwa. Siku ya Ijumaa tutawakumbuka raia wasio na hatia kama mashujaa kwa harakati dhidi ya haki ya uchaguzi katika eneo ambalo tutalitaja baadaye. Siku hiyo tutatangaza hatua tutakayochukua'', alisema kiongozi huyo wa upinzani.

Nasa, imesema inawataka maafisa wa polisi kusitisha mauaji hayo ambayo wamedai kuwa ni gharama kubwa kwa taifa.

''Serikali lazima isitishe ushirikiano wa maafisa wa polisi na majambazi mbali na ukiukaji wa kikatiba wa kuwapeleka polisi kuwakabili wafuasi wa NASA'', alisema.

Mapema leo Jumanne , Mahakama kuu ilisitisha kwa muda katazo la serikali dhidi ya maandamano ya IEBC katikati mwa miji ya Nairobi, Mombasa na Kisumu.
.

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari