Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Samaki wasababisha watano kufariki papo hapo

Wednesday , 15th Aug , 2018

Watu watano wamefariki dunia papo hapo na watatu kujeruhiwa, baada ya gari linalodaiwa kuwa lilikuwa likiwakimbia polisi kupinduka, ajali hiyo imetokea jana alfajiri eneo la Mika Kitongoji cha Bukwe wilayani Rorya mkoani Mara.

Pichani gari lililopata ajali.

Kamanda wa Polisi Tarime na Rorya, Henry Mwaibambe amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa ajali hiyo ilitokea wakati dereva aliyekuwa amepakia samaki wanaodaiwa kuvuliwa kinyume cha sheria akiwakimbia askari waliokuwa doria.

Baada ya ajali tulikuta mafurushi manne ya samaki yakiwa yameandikwa majina inaonekana ndio, watu waliokuwa wakipelekewa mizigo hiyo na zilichukuliwa na watu wa uvuvi kwaajili ya uchunguzi”, amesema Kamanda.

Mwaibambe amewataja waliofariki dunia kuwa ni mmiliki na dereva wa gari hilo, Athumani Masiaga (42) na Lucia Mwita (27) ambao wote ni wakazi wa Tarime mjini, wengine ni Mang’ala Baruti (40) na Jumanne Makonya (52), wakazi wa mji mdogo wa Shirati wilayani Rorya na Khadija Nangai ambaye umri na makazi yake hayajajulikana.

Kamanda Mwaibambe amewataja majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni Fidelis Fredrick (29), mkazi wa Busurwa wilayani Rorya; Mwita Saitoti (48) na Christina Nyangioso (28) ambao ni wakazi wa Tarime.

Mwezi  Februari mwaka huu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina kupitia oparesheni yake ya siku arobaini aliyoendesha katika mikoa ya kanda ya ziwa kupinga uvuvi haramu, alimwagiza katibu mkuu wa wizara hiyo anayeshughulikia uvuvi Dkt.Yohana Budeba pamoja na wakurugenzi wote wa halmashauri za wilaya katika mikoa ya kanda ya ziwa, kuwafuta kazi mara moja watumishi 65 na viongozi wa kamati za usimamizi wa raslimali za uvuvi (BMU) 26 baada ya kubainika wanashiriki kufadhili uvuvi haramu ndani ya ziwa Victoria.

HABARI ZAIDI

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma