
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba nchini Tanzania Deus Kibamba
Mwenyekiti wa jukwaa hilo Deus Kibamba amesema hatua ya kuwateua wawili hao inatokana na dalili za kukwama kwa mchakato wa katiba mpya, na hata kushindwa kupatikana kwa katiba yenyewe kama ilivyoahidiwa na Serikali kuwa ingepatikana kesho tarehe 26 April 2014.
Kibamba amesema ujuzi na uelewa wa watu hao katika usuluhishi na utatuzi wa migogoro, hususani ile ya kimataifa, utasaidia kupatikana kwa suluhu ya mgogoro unaotishia uhai wa harakati za katiba mpya nchini Tanzania.