Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali yafukuza wauguzi

Wednesday , 18th Apr , 2018

Serikali imewafukuza kazi wauguzi wote waliokuwa wanashiriki mgomo, baada ya kukataa kurejea kazini licha ya mwajiri wao kuridhia madai yao na kuwaongezea pesa, nchini Zimbabwe.

Katika taarifa iliyotolewa na Makamu wa Rais, Constantino Chiwenga imesema serikali imekerwa na imeona imedharauliwa kwa kiasi cha dola za Marekani 17,114,446 ambazo ni sawa na takribani 39 bilioni za Tanzania, kilichowekwa kwenye akaunti ya Wizara ya Afya ili kushughulikia malalamiko yao.

"Hii ilikuwa ishara ya nia njema ya serikali, uamuzi wa ghafla wa kuhamisha fedha katika mazingira haya magumu ya kiuchumi yanayoikabili nchi hayajaweza, kuwashawishi wauguzi kurejea kazini ili kuokoa maisha ya wagonjwa na kuwasaidia wagonjwa wanaohitaji msaada wao. Sasa inachukulia kwamba huu ni ukosefu wa huruma kwa vile wanachochewa kisiasa na pia ni kwenda kinyume cha masharti ya kazi na utumishi wa umma" amesema Makamu wa Rais Constantino Chiwenga

Tayari Rais Emmerson Mnangagwa ameidhinisha kufukuzwa kazi na kuhakikisha wauguzi wapya wenye mafunzo wanaajiriwa haraka iwezekanavyo ili waweze kuokoa maisha ya wagonjwa.

Manesi hao waliandamana kudai serikali kuwaongezea mishahara na kuboresha mazingira yao ya kazi, jambo ambalo serikali ya Zimbabwe iliamua kulitatua mara moja.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala