Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Tukimkuta mtu hana kitambulisho ni kosa" - Mwanri

Sunday , 10th Feb , 2019

Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri, amewataka wakuu wa Wilaya waliopo ndani ya mkoa huo kuhakikisha wanagawa vitambulisho vya wajasiriamali na kuwahimiza watu wengi zaidi kuchukua, wasipofanya hivyo basi wawatambue watu hao kuwa ni wavunjifu wa sheria.

Mwanri ametoa kauli hiyo alipokuwa akigawa vitambulisho vya wajasiriamali kwa wakuu wa wilaya mkoani humo, na kuwahimiza kwamba ni lazima wahakikishe wanawahimiza wahusika kuchukua.

Amewataka wakuu hao wa Wilaya kuwatafuta watu wasio navyo na kuwahoji wanafanya shughuli gani mjini, kwani watu wasiokuwa na shughuli yoyote huenda ndio watu wanaouvunja sheria na kuwaibia wengine.

Wapo watu watakaokwambia sina kazi, kataa mwambie hapa kazi tu, huna kazi kosa la pili, la kwanza nimekukuta huna kitambulisho, la pili umesema huna kazi, unaishi ishije, unakula wapi unalala wapi hapa mjini, tunataka uchukue kitambulisho, ili uende ukabangaize kwa ajili ya kutafuta chakula kwa watoto wako, uweze kupata nguo kwa ajili ya watoto wako”, amesema Mwanri.

Mwanri ameendelea kusema, “kwa hiyo tukimkuta mtu hapa mjini hana kitambulisho ni kielelezo kwamba hana shughuli yoyote ni kosa lingine, unambana, unamkuta hashughuliki lakini kavaa vuzuri, tunamuuliza unapata wapi mapato yako, tunajua huyu anaweza akawa muhujumu uchumi, au anapita nyumba za watu. Huna kitambulisho, hufanyi kazi, unaishi vizuri ni kosa lingine, unabambika makosa mpaka, wewe unaishi hapa mjini mtaa mmoja adi mwingine unadoea, kosa lingine, makosa karibu matano hapo”.

RC huyo pia amewasisitiza Wakuu hao wa Wilaya kuhakikisha fedha za kodi kwa wale wafanya biashara wasio na vitambulisho zinakusanywa ipasavyo, kwani wao ndio wawakilishi wa serikali kwenye maeneo yao.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala