Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Tumieni nguvu kazi ya wafungwa- Massauni

Sunday , 12th Aug , 2018

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhandisi Hamad Masauni amekabidhi mashine 10 za kufyatulia matofali kwa Jeshi la Magereza la mkoa wa Lindi na kuwataka kuzitumia ipasavyo ili kukabiliana na changamoto zinazowakabili ikiwemo makazi duni.

Mkuu wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Lindi, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Rajabu Nyange, akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), baada ya kupokea mashine 10 za kufyatulia tofali ambapo ni mpango maalumu wa serikali kuondoa changamoto za makazi ya askari magereza nchini. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi,Shaibu Ndemanga.

Mashine hizo ni sehemu ya ahadi aliyoitoa mwaka mmoja na nusu uliopita baada ya kufanya ziara katika mkoa huo na kukutana na changamoto mbalimbali ikiwemo makazi duni ya nyumba za udongo hasa katika gereza la Lindi mjini.

Aidha, Mhandisi Masauni amewataka wakuu wa Jeshi la Magereza mkoani humo kujipanga ipasavyo namna ya kuzitumia machine hizo ili ziwe na tija na manufaa kwao.

"Nawakabidhi mashine hizi, natarajia kuona mabadiliko yenye tija kutoka kwenu, mkifanya vizuri nitawatafuta wadau wengine kwa ajili ya kuongeza mashine hizi. Nataka gereza la Lindi Mjini liwe la mfano kwa magereza ya mkoa huu. Tumieni nguvu kazi ya wafungwa mlionao kwa ajili ya kuboresha makazi yenu", amesema Masauni.

Hata hivyo, Masauni amesema ana matumaini makubwa na magereza katika kukabiliana na changamoto mbalimbali na kuzitumia mashine hizo kwa ufanisi mkubwa ili wapate makazi bora kwa manufaa ya askari na maofisa wao.
 
Kwa upande wake, Mkuu wa Magereza ya Mkoa wa Lindi (RPO), Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Rajab Nyange amemshukuru Mhandisi Masauni kwa msaada huo alioutoa kwa kile alichokielezea kuwa hali ya makazi ya askari wa jeshi hilo siyo nzuri

Naye, Mkuu wa gereza la Lindi Mjini (SP), Emanuel Pagali amesema mashine hizo ni nzuri na zitawasaidia kwa utekelezaji wa majukumu yao ikiwemo kuboresha makazi ya maofisa na askari wa jeshi hilo

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi