Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vigezo vya mikopo chuo kikuu vyazua gumzo

Wednesday , 16th May , 2018

Zikiwa zimepita takribani siku 6 tokea kulipofunguliwa dirisha la uombaji mikopo kwa njia ya mtandao nchini, wanafunzi na wadau mbalimbali wameendelea kuilalamikia Bodi ya Mikopo kwa kuweka vigezo vigumu bila ya kuwafikilia kwa undani watu wanaotaka kufaidika nayo.

Akizungumza kwenye kipindi cha EATV Saa1 Katibu Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP), Joseph Malecela amesema katika utoaji wa mikopo hiyo kumekuwa na ubaguzi wa upendeleo kwa baadhi ya michepuo ya wanafunzi hasa hasa wanaosomea sayansi huku wengine wakikosa kabisa.

Mbali na hilo, Malecela amesema ni vyema Bodi ya Mikopo itoe ufafanuzi zaidi juu ya kifungu cha muongozo wa kuomba Mkopo Na 1.0 (vii) ambacho kinasema 'waombaji ambao wazazi au walezi ni wamiliki wa biashara, mameneja wakubwa katika mamlaka zinazotambulika zenje usajili, hawaruhusiwi kuomba mkopo'.

"Sisi tunachojiuliza kama Mtandao wa wanafunzi Tanzania kwamba tuna mfumo gani wa mkopo ambao unaweza kupima kiwango cha uwezo wa mzazi katika kuweza kumudu hizo gharama, na madodoso gani yamewekwa ili kujua huyu mtu anafanya biashara kubwa hata kama si Meneja mkubwa", amesema Malecela.

Kwa upande wake Afisa Mawasiliano Mwandamizi kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Bi. Veneranda Malima amesema kifungu hicho kipo sawa na hawawezi kusema kwamba kitaondolewa.

Sikilize hapa chini mjadala mzima kupata kufahamu maana halisi ya kigezo cha leseni kilichoweza kuzua gumzo kila mahali.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ