
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo) Zitto Kabwe.
Zitto kupitia ukurasa wake wa twitter amesema kuwa Rais pia awasikilize kuhusiana na madai ya wadau wa korosho pamoja na kero nyingine na asiishie kwenye kikokotoo cha mafao ya hifadhi ya jamii pekee.
"Rais Magufuli atusikilize pia kuhusu mishahara ya watumishi wa umma, atusikilize kuhusu mateso ya wadau wa korosho na atusikilize kuhusu muswada wa sheria ya vyama vya siasa", ameandika Zitto Kabwe.
Zitto ameongeza kuwa, "Kwetu huu si wakati wa kunyang'anyana sifa. Washindi ni wafanyakazi na Watanzania. Tunapoelekea mbele, tunamuomba Rais Magufuli asiwe na aibu kutusikiliza na mengine mengi kwa kuwa nia yetu ni njema tunajenga nchi moja".
Mapema leo Rais Magufuli, ameagiza vikokotoo vya mafao ya wafanyakazi katika mifuko ya hifadhi ya jamii, vilivyokuwa vinatumika kabla ya mifuko kuunganisha viendelee kutumika kwa kila mfuko hadi mwaka 2023.