
Rais wa Kenya (Kushoto),Uhuru Kenyatta akisalimiana na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma
Msemaji wa Ikulu ya Kenya Monoah Esipisu amesema jana kuwa Rais Uhuru Kenyatta atatumia ziara hiyo ya Rais Zuma kutaka kuwepo mazingira mazuri ya viza kwa wakenya.
Mapema mwaka huu, Kenya ilikuwa ikishinikiza kuondolewa kwa gharama za sasa za viza zinazotozwa raia wake wanapoingia kwenye viwanja vya ndege vya Afrika Kusini.